Website ya ya st francis university college of health and allied science (SFUCHAS) imedukuliwa (hacked) na wadukuzi kutoka Algeria.
TUNAKUPATIA HABARI ZA BIASHARA MICHEZO AFYA SIASA NA BURUDANI NA MAHUSIANO TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KUPITIA 0657191827,0753127275,0789930603
Wednesday, 20 July 2016
Tuesday, 19 July 2016
HATIMA YA WANAFUNZI WALIOFUKUZWA UDOM IKO HAPA
Serikali iliwarejesha nyumbani wanafunzi 7,805 waliokuwa wanasoma Stashahada Maalum ya Ualimu wa Sayansi na Hisabati Chuo Kikuu Dodoma.
Wanafunzi waliosimamishwa masomo walikuwa wamegawanyika katika makundi makuu mawili. Kundi la kwanza lilikuwa ni wanafunzi 6,595 waliodahiliwa katika Stashahada Maalumu ya Ualimu wa Elimu ya Sekondari na kundi la pili lilikuwa na wanafunzi 1,210 waliodahiliwa katika mafunzo ya Stashahada ya Ualimu wa Elimu ya Msingi.
Taarifa iliyotolewa leo na waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Joyce Ndalichako amesema kwamba baada ya hatua ya kuwaondoa wanafunzi chuoni kuchukuliwa, Serikali ilifanya Uchambuzi wa wanafunzi hao kwa lengo la kujiridhisha na sifa zao. Baada ya uchambuzi huo leo July 19 2016 Serikali imetangaza maamuzi haya…….
Kundi la Stashahada Maalumu ya Ualimu wa Elimu ya Sekondari
Serikali imesema kwa kuwa uchambuzi umebainisha kuwa Wanafunzi wenye ufaulu wa Daraja la I na la II ambao pia wamefaulu masomo mawili ya Sayansi kwa kiwango cha C-A ni 382 (mwaka wa I -134 na mwaka wa II – 248), wanafunzi hao ndiyo pekee watakaorudishwa katika Chuo Kikuu cha Dodoma ili wakamalizie mafunzo yao katika Chuo hicho.
Wanafunzi 4,586 wa mwaka wa I wa Programu Maalum ya Stashahada ya Ualimu wa Elimu ya Sekondari waliokidhi vigezo vya ufaulu watahamishiwa katika Vyuo vya Ualimu vya Morogoro, Butimba, Mpwapwa, Songea na Tukuyu kuendelea na masomo yao.
Wanafunzi 1,337 wa Mwaka II watahamishiwa kwenye Vyuo vya Ualimu vya Korogwe na Kasulu kumalizia masomo yao.
Wanafunzi 290 waliokuwa wamedahiliwa kusoma Programu Maalum ya Stashahada ya Ualimu wa Elimu ya Sekondari Masomo ya Sayansi na Hisabati ambao hawana sifa stahiki wanashauriwa kuomba mafunzo yanayolingana na sifa walizo nazo kwenye chuo chochote wanachotaka wao.
Kundi la Programu ya Ualimu wa Elimu ya Msingi
Serikali imesema wanafunzi katika kundi hili hawakuwa sehemu ya program maalum ya kupunguza uhaba wa walimu wa Sekondari wa Sayansi na Hisabati. Walikuwa wanaandaliwa kufundisha shule za msingi wakati lengo la Programu Maalum ilikuwa ni kukabiliana na tatizo za uhaba wa walimu wa Sekondari. Maudhui ya program waliyokuwa wanasoma hayakuwa sawasawa na yale ya Programu ya Ualimu wa Sekondari wa Sayansi na Hisabati.
Wanafunzi 29 wa mwaka wa II wenye Cheti cha Daraja IIIA waliodahiliwa kusoma Stashahada ya Ualimu wa Shule za Msingi watahamishiwa katika Chuo cha Ualimu Kasulu wamalizie masomo yao kwa gharama zao wenyewe.
Wanafunzi 1,181 waliodahiliwa kusoma Stashahada ya Kawaida ya Ualimu wa Elimu ya Msingi waombe mafunzo yanayolingana na sifa walizonazo mahali popote watakapotaka wao.
Aidha Serikali imesema itaendelea kuwapatia mikopo wanafunzi watakaorejeshwa UDOM na wanafunzi watakaohamishiwa kwenye Vyuo vya Ualimu vya Serikali watapewa mkopo wa kiasi cha Sh. 600,000/= kwa mwaka ambayo ni ada ya Mafunzo ya Ualimu itakayolipwa moja kwa moja Chuoni.
Monday, 18 July 2016
Mmarekani Mweusi awaua Polisi 3 wa kizungu
Mshirikishe mwenzako

Rais Barrack Obama wa Marekani amewasihi wamerakani wajizue dhidi ya hisia kali baada ya Mmarekani Mweusi kuwapiga risasi na kuwaua maafisa watatu wa polisi katika shambulizi la pili la kulipiza kisasi dhidi ya polisi wazungu wanaowaua wamarekani weusi.
Obama ameomba uvumilivu utawale mioyo ya wakaazi wa mji wa Baton Rouge Louisiana nchini Marekani ambao sasa wanahofu ya kuzuka mashambulizi ya kulipiza kisasi.

Obama aliyasema hayo katika hotuba ya moja kwa moja kupitia kwa runinga kutoka ikulu ya WhiteHouse muda mchache tu baada ya mtu mmoja mweusi kuua maafisa watatu wa polisi hukohuko Baton Rouge alikouawa mtu mweusi
Alton Sterling pasi na hatia yeyote majuma mawili yaliyopita.

Hasira imekuwa ikitokota miongoni mwa watu weusi baada ya mtindo wa kuuawa kwa wanaume weusi na polisi wazungu kuendelea kwa muda mrefu ilihali hakuna hatua inayochukuliwa dhidi yao.
Gavin Long ambaye ni mwanajeshi wa zamani alikuwa amerekodi ujumbe katika mji wa Dallas siku chache baada ya polisi watano kuuawa mjini humo katika shambulizi lililotekelezwa kulipiza kisasi cha mauaji ya Sterling.

Sasa imebainika kuwa Long alikuwa ameweka video kwenye mtandao akilalamika jinsi polisi wanavyowatendea waamerika weusi ambapo alitoa wito kwa wanaume weusi kujitolea kuokoa jamii yao.
Long mwenye umri wa miaka 29 aliwahi kuhudumu kama mwanajeshi wa Marekani .
Rais Obama ameshauri watu weusi dhidi ya kutekeleza mashambulizi dhidi ya Polisi akisema mauaji ya kulipiza kisasi sio suluhisho la tatizo sugu la ubaguzi wa rangi bali utachochea uhasama zaidi dhidi yao na polisoi wazungu
Friday, 15 July 2016
JIFUNZE KUWA NA SHUKRANI
Alimpenda mno mke wake, alijitahidi kumpa mkewe kila kitu kilochopo ndani ya uwezo wake, lakini mke wake hakuwa akiridhika na ku appriciate. Ingawa hakuwa tajiri lakini alijitahidi mno ku share kile alichonacho.
Kila alipomnunulia nguo mkewe, jibu pekee alilolipata lilikuwa ni kwamba alikuwa akikamilisha jukumu lake kama mume. Mkewe hakuwahi kutoa shukrani hata mara moja.
Mwanaume angemnunulia nguo mkewe lakini mkewe alikuwa akimjibu kwamba nguo ni ya bei ya chini na u quality yake ni ndogo. Mume angetabasamu na kumwambia mkewe kwamba "siku moja nitakapokuwa tajiri nitakununulia vitu vyote vya gharama unavyovitaka" kwa sasa naomba nivumilie tu mke wangu!
Mke hakuwa akimpigia simu mume wake labda tu pale alipokuwa akihitaji kitu au pesa kutoka kwa mumewe, na kama asipokamilishiwa ombi lake ilikuwa ni ugomvi kwa siku kadhaa.
Jioni moja, mume alirudi kutoka kazini, alileta nyumbani kilogramu moja ya nyama, kwa furaha tele alitegemea kumsuprise mkewe. Alifika nyumbani na kumuona mkewe na akamuonyesha ile kilo ya nyama! Mkewe kwa dharau akamwambia " eh na ndio unajiita mwanaume? Unafikiri kurudi nyumbani na kilo moja ya nyama bila viungo, mafuta ya kupikia wala mbogamboga ndio kutakufanya uonekane kidume? Bora ungeacha tu! Huna msaada wowote hapa.
Kisha akaenda kuitupa ile nyama jalalani, mume alijisikia vibaya sana lakini hakuchoka kuendelea kumpenda mkewe. Aliendelea kufanyiwa vituko mbalimbali lakini hakuteteleka juu ya mapenzi kwa mkewe na familia yake.
Siku moja mume alipatwa na maumivu ya mguu wa kushoto, baadae uvimbe ukatokea katika mguu na ukawa ukikua siku baada ya siku.
Alienda hospitalini na akakutwa alikuwa na kansa, hakuwa na pesa za kutosha za matibabu ya kansa. Japo alikuwa mgonjwa ila alijitahidi kuhudumia familia yake.
Miaka miwili baadae hali ilizidi kuwa mbaya, mpaka akapelekwa katika chumba cha wagonjwa mahututi. Alifanyiwa operation na mguu ukaondolewa baada ya kuwa umeathiriwa vibaya na kansa. Lakini kwa bahati mbaya walikuwa wamechelewa, ugonjwa ulikua umesha athiri na maeneo mengine mengi ya mwili.
Alimwita mkewe na kumwambia "NITUNZIE WANANGU" najihisi mwili udhaifu, roho inataka kunichomoka, maumivu hayaniishi, nafikiri siwezi kuishi tena! Siku zote nitakuwa na wewe kiroho! Mwenyezi Mungu akubariki na ninakupenda sana mke wangu!
Alivuta pumzi yake ya mwisho na kufariki. Mkewe na watoto wake pamoja na ndugu na marafiki waliomboleza msiba ule na wakazika!
Miezi mitatu baadae mkewe alikuwa ameinamia kaburi la mumewe akitamka maneno haya kwa uchungu mwingi!
"Mume wangu mpenzi! Ulifanya kila uwezalo kunihudumia, ulinijali vema na kunipa kile kilichokuwa ndani ya uwezo wako. Ila mimi nilichokulipa ni migogoro na ugomvi usiokwisha. Sikutambua umuhimu wako! Nimeuona sasa hivi ulivyoondoka na kuniachia watoto!
Sasa nimekua mimi ndio wa kuwatafutia chakula watoto, kuwalipia ada, mavazi na kila kitu! Sio siri ulikuwa wa muhimu sana
Nakumbuka siku ile nilivyotupa jalalani ile kilo ya nyama, lakini sasa sijui hata kilo moja ya nyama naipata wapi.
Wema hufa mapema! Najuta mume wangu, mume ambae kila nilipokuudhi hukuonesha kukasirika bali ulitabasamu. Najua unanisikiliza nakuomba sana unisamehe. Wote tumekumbuka uwepo wako. Mwanao Diana kila siku anauliza utarudi lini?
Hautatutoka akilin mwetu mpaka pale tutakapoungana na wewe huko uliko. Mwenyezi Mungu akulaze mahala pema peponi.
MUHIMU:
*Siku zote kubali kile ulichopewa bila kujalisha ni kidogo ama kikubwa.
*Mapenzi sio ni nini tulicho nacho, au ni utajiri gani tulionao ila mapenz ni ku share kile kidogo tulicho nacho
*Ushawahi kuchukua muda wako na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kile alichokubariki nacho? Kama hujawahi kufanya hivyo ni bora ufanye sasa!
Shukuru Mungu kwa alichokupa, kitunze kidumu. usije ukajikuta ukipoteza almasi wakati upo busy ukikusanya mawe.
Wednesday, 13 July 2016
Vituko vya Museveni Mshirikishe mwenzako

Je ushawahi kupokea simu ya dharura? Je wewe hujitenga vipi na watu waliokaribu nawe ima ni mkeo ama hata wafanyakazi wenza ili upokee simu ya kibinafsi?
Na je katika enzi hizi za simu za kisasa au Smartphone wangapi wetu wanatumia simu za kale zisizo na touchscreen?
Haya basi, Hayo sio maswali ya kipima joto ... la!

Rais wa Uganda Bw Yoweri Kaguta Museveni alizua kioja katika kijiji cha Kyeirumba, wilaya ya Isingiro karibu na mpaka wa Uganda na Tanzania aliposimamisha msafara wake wa magari ili apokee simu "ya dharura". Picha za kisa hicho zilipakiwa kwenye mtandao wa Facebook na afisa wake wa habari Don Wanyama.
Amini usiamini Rais Yoweri Museveni, alishuka kutoka kwenye gari lake rasmi akachukua kiti chake na kukiweka kando kando ya barabara mpya ya Isingiro ikipitia kijiji hicho cha Kyeirumba hadi Tanzania na kupokea simu faraghani.

Mzee Museveni kama vile baba wa taifa alitumia muda wake kufanya shughuli hiyo huku akiwapungia mkono wapita njia.
Baada ya dakika 30 hivi raia wa kijiji hicho walishangaa kuwa miongoni mwa maafisa wakuu serikalini.

Ilikuwa ajabu sana kwao kumuona Museveni akiwa ameketi barabarani.
Waganda katika mitandao ya kijamii wamesambaza picha hiyo ya rais museveni akizungumza kwa simu ambayo inaonekana kuwa sio ya kisasa.

Wengine wanamkejeli kwa kuhofia kudukuliwa huku wengine wakimkosoaa kwa kuketi barabarani.
''Kwani hangeweza kupokea simu yake ndani ya gari lake?"
''Ni siri gani hiyo ambayo hakutaka hata walinzi wake wasikie.
''Ama ilikuwa ni #Besigyexit?", wakizungumzia kuachiliwa kwa dhamana kwa kiongozi wa upinzani Dkt Kizza Besigye mapema asubuhi
Tuesday, 5 July 2016
Mtoto mnene zaidi duniani
Arya Permana
Mtoto wa miaka 10 kutoka Indonesia, ambaye ametajwa kuwa mtoto aliyenenepa zaidi duniani ameanza kupewa chakula cha kupunguza uzani kwa kuwa wazazi wake wanahofia afya yake.
Arya Permana ana uzani wa kilo 188 na ameorodheshwa kuwa na unene usio wa kawaida.
BBC ilizungumza na mamaake Rokayah huko Karawang Indonesia ambaye ana wasiwasi sana kuhusu afya ya mwanawe.
Monday, 20 June 2016
Al shabaab waua polisi 5 Mandera Kenya
Mshirikishe mwenzako
Maafisa 5 wa polisi wa Kenya wameuawa mapema leo mjini Mandera katika shambulizi lililotekelezwa na wapiganaji wa kundi la wanamgambo la Al shabab kutoka Somalia.
Kamishna wa jimbo hilo la kaskazini mashariki mwa Kenya bwana Job Borongo ameithibitishia BBC kuwa wapiganaji hao walifanya shambulizi la kuvizia dhidi ya msafara wa magari ya polisi uliokuwa ukienda El Wak wakitumia guruneti.
Maafisa hao tano waliangamia papo hapo huku gari walimokuwa wakisafiria likiharibiwa kabisa.
Maafisa wengine wanne wamejeruhiwa vibaya.
Msafara huo wa polisi ulikuwa ukitoa ulinzi kwa msafara wa mabasi ya uchukuzi wa umma, desturi iliyoanzishwa baada ya wapiganaji hao kuteka basi moja na kuua abiria 28 wakristu.
Gavana wa Mandera bwana Ali Roba aliwalaumu maafisa wa polisi katika eneo hilo kwa kupuuza tahadhari iliyotolewa na wenyeji kuhusiana na mashambulio ya kigaidi.
Roba anasema walipuuza vyanzo vya kiintelijensia vilivyotolewa kuhusiana na kuonekana kwa wapiganaji hao waliojihami.
Hii si mara ya kwanza Mandera kushuhudia mashambulizi ya al shabaab.
Shambulizi hilo la Novemba mwaka wa 2014 liliwaacha wasafiri wengi wasiokuwa waislamu na hofu ya kusafiri na hivyo kuilazimu serikali kutoa usalama kwa mabasi ya uchukuzi wa umma.
Mwezi mmoja baadaye wapiganaji hao waliwaua wachimba migodi 36 katika eneo hilo la Mandera.
Kundi hilo la wapiganaji wa kiislamu limekuwa likitekeleza mashambulizi katika maeneo ya kaskazini mwa Kenya likitaka kuishinikiza taifa hilo jirani kuondoa majeshi yake nchini Somalia.
Kenya ilipeleka vikosi vyake vya jeshi nchini Somalia mwaka wa 2011 ikitaka kuzima mashambulizi ya mara kwa mara.
Hata hivyo kundi hilo limeongeza mashambulizi nchini kenya ikiwemo mauaji ya watu 67 katika maduka ya Westgate mjini Nairobi mwaka wa 2013.
Mwaka uliopita Al Shabab ilitekeleza mashambulizi katika chuo kikuu cha Garissa na kusababisha vifo vya wanafunzi 148
Subscribe to:
Posts (Atom)