Friday, 15 September 2017

Tanzania yashangazwa na uchunguzi wa UN kuhusu Korea Kaskazini




Dkt Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje, Tanzania
Tanzania imesema imeshtushwa baada ya kuorodheshwa miongoni mwa nchi ambazo zimechunguzwa na Umoja wa Mataifa na kuhusishwa kuwa na uhusiano wa kibiashara na Korea Kaskazini.
Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, waziri wa mambo ya nje Dkt. Augustine Mahiga, amesema licha ya uhusiano uliokuwepo awali, lakini tangu mnamo mwaka 2014, Tanzania imepunguza kabisa uhusiano wa kibiashara na kidiplomasia na nchi hiyo.
"Hatuna ugomvi na Korea Kaskazini,lakini kitendo chao cha kutengeneza masilaha ya kuangamiza sio mazuri kwa heshima na usalama duniani.Ndiyo maana tukaanza kuchukua hizo hatua za kupunguza mahusiano." amesema Dr Mahiga kwa waandishi wa habari leo.
Waziri Mahiga ameongeza kusema kuwa, uhusiano huo wa kibiashara ulikuwepo kabla ya vikwazo vilivyowekwa hivi karibuni na Baraza la Umoja wa Mataifa.
Waziri huyo amesema anaelekea katika mkutano wa kawaida wa Umoja wa Mataifa, ambapo atatumia fursa hiyo kujibu tuhuma hizo kwa Baraza la Usalama.
Tanzania na Uganda ni miongoni mwa baadhi ya nchi zinazochunguzwa na Umoja wa Matiafa kwa tuhuma za kwenda kinyume na vikwazo vilivyowekwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi ya Korea Kaskazini.
Ripoti ya uchunguzi huo ilitolewa mnamo tarehe 9 mwezi wa Septemba. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema linachunguza tuhuma za Tanzania kuingia mikataba ya kijeshi na Korea Kaskazini inayogharimu dola za kimarekani milioni 12.5

MTANZANIA ALIYEFANIKIWA KUJIUNGA PSG MWAKA HUU


Saturday, 26 August 2017

Jeshi la Polisi Arusha lazuia mikutano ya Lema





Arusha. Jeshi la polisi mkoani Arusha, limepiga marufuku mikutano ya mbunge wa jimbo la Arusha mjini (Chadema), Godbless Lema iliyokuwa inaendelea katika jiji la Arusha ili kupisha maandalizi ya mtihani wa darasa la saba na mbio za Mwenge.
Katika barua ya Mkuu wa polisi wilaya ya Arusha, Mrakibu mwandamizi wa polisi (SSP),E.Tille ambayo imethibitisha na Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha,(SACP) Charles Mkumbo imeeleza kuwa, Lema amezuiwa kufanya mkutano kuanzia kesho Agosti 27 hadi Septembaa mosi.
"Ofisi ya Mkuu wa polisi wilaya ya Arusha, inakutaarifu kuwa imezuia mikutano yako yeye ratiba kuanzia Agosti27 hadi Septema mosi kwa ajili ya kupisha maandalizi ya kuhitimisha mtihani wa darasa la saba na mwenge wa uhuru" ilisomeka barua hiyo na kushauri Lema kupanga mikutano kuanzia Septemba 8 mwaka huu.
Kamanda Mkumbo amesema, sababu kubwa ya kuzuiwa mikutano hiyo ni kwa kuwa wanahitajika polisi wa ulinzi na hivyo haiwezekani kupata polisi wa kulinda mikutano na pia kushiriki katika masuala ya mitihani na mwenge.
"Haya ni mambo ya kitaifa hivyo ndio sababu OCD amesitisha mikutano ya mbunge na mambo haya yakimalizika ataendelea na mikutano yake"alisema.
Akizungumza na mwananchi jana, Lema alisema anapinga polisi kuzuia mikutano yake, kwani ni ukiukwaji wa sheria na haki za mbunge.
Lema amesema sheria ya bunge kifungu cha  nne fasihi ya  kwanza, kinazungumzia uhuru wa mbunge kufanya mikutano jimboni kwake na kifungu cha 4(1) na (2) vinaelezea uhuru huo wa mbunge kufanya mikutano na pia ni ukiukwaji wa sheria kuzuia mikutano ya mbunge kwenye jimbo lake.
Lema amesema anaamini, kuzuiwa mikutano yake ni njama baada ya kubainika katika mikutano zaidi ya  10 ambayo amefanya katika jimbo la Arusha imekuwa na mafanikio makubwa na wananchi wa Arusha wamepata fursa ya kujua ukweli wa mambo mbali mbali.
"Hizi ni njama najua walipanga kuvuruga mikutano na kuharibu vyombo vyangu wakashindwa, wakanitakama kwa kuzidisha dakika 7 kwenye mkutano wangu mmoja nikawashinda kwa hoja sasa wameona wazuie kabisa na ikiwezekana watumie nguvu"alisema
Amesema sasa anashauriana na wanasheria wake kuona kama akubali barua ya polisi ama aendelee na mikutano kwani kimsingi, maeneo ambayo mikutano imepangwa kufanyika sio ya shule .
"Sasa kesho Jumapili nipo nje ya mji eneo la Olmoti kuna maandalizi yapi ya mwenge na darasa la saba , ntakuwa na mkutano eneo la soko la Shuma kuna mkusanyiko kila siku wa watu, nitaathiri nini huo mwenge ambao utafika kuanzia Septemba 6"amesema
Hata hivyo amesema, baada ya barua hiyo na  kushauriana na mawaziri kadhaa na viongozi wa serikali, atalifikisha pia bungeni, kwani ni jambo la ajabu mbunge kuzuiwa kufanya mikutano kwasababu za mwenge na mitihani ya darasa la saba.
Amesema muda ambao umetakiwa na polisi afanye mikutano, anapaswa kuwa katika shughuli za kibunge jambo ambalo anaamini litaathiri ratiba za utendaji wa kazi zake.

MAN U VS LEICESTER CITY


Wednesday, 2 August 2017

FAITHFULLNES-KISA KIZURI CHA KUSISIMUA.



F A I T H F U L N E S S .
Alikuwa bafuni akioga...
"Honey, mama yako anakupigia..anataka umtumie pesa uliyomwambia mapema" Mkewe akawa akimwambia mumewe huku akiwa chumbani
"Sawa wife, naomba nisaidie ingia kwenye menu ya M-PESA kwenye simu yangu na mtumie shilingi laki moja" Mume akaongea kwa nguvu kutoka bafuni.
Mke akastaajabu. Inakuaje kirahisi rahisi hivyo Mumewe anamuamini na account yake ya MPESA.
"Baby, simu yako umeweka password. Mimi sijui password yako" mke akashauti tena kumwambia mumewe aliyepo bafuni...
"Password ya simu ni 2789. Na passowrd ya MPESA ni hiyo hiyo 2789" Mume nae akamjibu mkewe kutokea bafuni..
Akachukua simu ya mumewe, akaingiza password 2789 na simu ikawa unlocked. Akamtumia mama mkwe wake shilingi laki moja kama alivyoambiwa na mumewe.
Baada ya kutuma, akaingiwa na tamaa ya kupitia pitia sms kwenye simu ya mumewe. Akajiuliza maswali, kwanini mumewe aweke Password kwenye simu yake? Anaficha nini?
Akiwa anaangalia angalia chats mbalimbali facebook, WhatsApp na sms za kawaida kwenye simu ya mumewe hakuamini macho yake...
Chats nyingi zilionesha mumewe akimzungumzia yeye vizuri kwa marafiki zake na familia yake, aliona sms nyingine mumewe akimsifia hata mbele ya wanawake wengine...
Mke akatabasamu na kujawa na uso wa furaha baada ya kuona mumewe kwa kiasi gani anamjali. Akaona ni kwa kiasi gani mumewe yupo upande wake akimpigania..
Akaona baadhi ya wanawake waliokuwa wakimtumua sms za kiuchokozi chokozi jinsi walivyomwagwa, na baadhi yao aliona mumewe amewatumia picha yao ya pamoja na kuandika caption kwamba "Huyu ndiyo mwanamke nimpendae" Kitu ambacho kiliwaziba midomo wanawake wengine..
Kadiri alivyozidi kupekua simu ya mumewe ndivyo alivyozidi kugundua ni kwa namna gani mumewe ni rafiki mzuri kwa watu. Anao marafiki wengi kwenye chat list yake na marafiki wa kweli wakizungumza dili za maana..anapendwa na wengi na wanamkubali..
...Akaona ni kwa kiasi gani mumewe anawaombea watu, akiwaandikia sala na akiwabariki..akaona sms za kuwatia moyo wale waliokuwa wakimuandikia issue zozote za ushauri..
...Huyu mume wake ni wa ajabu, mume muaminifu, rafiki wa kweli, ndugu mwajibikaji kwa ndugu na wazazi wake, na mzungumzaji mzuri ambapo watu wengi wanapenda kuongea na kuchat nae..
..Mke akajisikia vibaya kwa hapo mwanzo kuwaza kwamba mumewe sio muaminifu jambo ambalo si kweli.
"Umeshamtumia mama pesa?" Mumewe akamuuliza huku akitoka bafuni akiwa amejifunga taulo.
"Ndio babylove..njoo hapa mpenzi wangu" Mke akamwambia mumewe huku akiinuka kitandani na kuweka simu pembeni.
Akamkumbatia mumewe kwa nguvu..
Akambusu kwa hisia kali. Uaminifu unampa raha mwanamke.
Akamvua taulo mumewe. Akamsukuma kitandani na kuanza kukanda kanda mwili wa mumewe..
"Oh baby, inaonesha una njaa na mimi eeh" Mume akaongea huku akisikilizia raha ya kupapaswa na mikono laini ya mkewe jambo lilofanya hisia zake ziamke.
Mke akakaa juu ya mumewe na wakafanya lile tendo lililoidhinishwa kwao...naam tendo la ndoa.
"Nakupenda sana swewtheart" mke akamwambia mumewe baada ya kumaliza mtanange.
"Nakupenda pia Darling". Mume akamjibu mkewe huku akimbusu kwenye paji la uso.
Siku chache baadae, alipomuuliza mumewe kwanini ameweka password kwenye simu yake, mumewe alimjibu kuwa ameweka password kwa sababu ya usalama wa nyaraka zake na pia kulinda usiri wa zile chats hot ambazo wamekuwa wakichat pamoja kama mke na mume. Kwamba watu wengine wasipate kuona maongezi yao.
Mke akakumbuka mambo ya kikubwa waliyokuwa wakichat na mumewe hasa pale anapokua mbali nae na akaona mantiki ya mumewe kuweka password kwenye simu yake.
______________________________
Usiwe mwepesi sana kumhisi mpenzi wako vibaya. Sio kila mtu ni msaliti kwenye ndoa yake. Kuna watu wako serious na mahusiano yao. Kwa sababu usaliti ni maamuzi ya mtu binafsi na wala sio bahati mbaya.
"Cheating is hard work. You gotta keep deleting text, keep locking your phone, keep deleting messages off of facebook, twitter, whatsap and think of lies..that's too much! rather be loyal"
Blessed .