Wednesday, 28 March 2018

Ureno 0-3 Uholanzi: Cristiano Ronaldo apigwa breki mjini Geneva

 


Cristiano RonaldoHaki miliki ya pichaEPA

Mabingwa wa Ulaya Ureno walipokezwa kichapo cha kushangaza na Uholanzi katika mechi ya kimataifa ya kirafiki iliyochezewa mjini Geneva, Uswizi.
Winga wa zamani wa Manchester United Memphis Depay na mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Ryan Babel waliwaweka Waholanzi 2-0 mbele.
Beki wa Uholanzi Virgil van Dijk, ambaye majuzi alitawazwa nahodha mpya wa timu hiyo, alifunga la tatu.
Mchezaji wa Ureno Joao Cancelo alipewa kadi nyekundu dakika ya 61 baada ya kupokezwa kadi ya pili ya manjano.

Cristiano RonaldoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionCristiano Ronaldo alikuwa amefunga mabao mechi nane mfululizo kabla ya mechi hiyo

Katika mechi hiyo, mkimbio wa kufunga mechi nane mtawalia wa mshambuliaji nyota wa Ureno anayechezea Real Madrid Cristiano Ronaldo ulifikishwa kikomo.
Nahodha huyo wa Ureno aliondolewa uwanjani dakika ya 68 na nafasi yake akaingia kiungo wa Monaco Joao Moutinho.
Ronaldo alikuwa amefunga mabao 17 akichezea Real na mawili akichezea Ureno dhidi ya Misri Ijumaa katika kipindi hicho alichofunga mabao mechi nane mtawalia.

Kundi B

Ureno wamo Kundi B katika Kombe la Dunia pamoja na Uhispania, Morocco na Iran.
Lakini Uholanzi, ambao walishindwa 1-0 na England mechi ya kwanza Ronald Koeman akiwa mkufunzi wao, hawakufuzu kwa michuano hiyo itakayoanza mwezi Juni.

Messi kurejea dimbani

Kwingineko, Lionel Messi anapangiwa kurejea uwanjani kuwachezea Argentina mechi ya kirafiki dhidi ya Uhispania Jumanne.
Hakucheza mechi ambayo walilaza Italia 2-0 mjini Manchester Ijumaa kutokana na jeraha la misuli, lakini ameimarika na kuruhusiwa kuchezea taifa lake mjini Madrid.
Kocha wa Argentina Jorge Sampaoli amesema Messi alifanya mazoezi kama kawaida Jumatatu.

Argentina's Lionel Messi and Sergio AgueroHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionLionel Messi amepona jeraha la misuli lakini mwenzake Sergio Aguero bado hawezi kucheza

Nyota huyo wa Argentina huenda akacheza dhidi ya wenzake wa Barcelona wanaochezea timu ya Uhispania Gerard Pique na Jordi Alba.
Uhispania walitoka sare 1-1 na Ujerumani mjini Dusseldorf Ijumaa, na kuendeleza mkimbio wao wa kutoshindwa chini ya Julen Lopetegui hadi mechi 17

Wednesday, 7 March 2018

Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) adaiwa kutoweka Katika mazingira Ya Kutatanisha

Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) umesema mwenyekiti wake Mahmud Abdul Ormari Nondo hajulikani alipo na kulitaka jeshi la polisi kuhakikisha anapatikana akiwa salama kwa haraka.
Baba mdogo wa kiongozi huyo Mussa Mitumba akiwahutubia wanahabari pia ametoa wito kwa 'mwanawe' kurudishwa akiwa hai aendelee na kutafuta kutimiza ndoto zake.
Kiongozi huyo wa wanafunzi alionekana mara ya mwisho mnamo Jumanne katika afisi za shirika hilo eneo la Sinza, Dar es Salaam alipokuwa akitoa ufafanuzi kuhusu taarifa iliyokuwa imetolewa na shirikisho la vyuo vikuu nchini humo, Tahliso.
Muungano huo unasema baada ya kuondoka afisi hizo, Bw Nondo alielekea chuoni na kuaga kuwa anaondoka kwenda nyumbani Madale.
"Ghafla katika hali ya kutatanisha, kuanzia saa 6 hadi saa 8 usiku alijitoa kwenye makundi yote ya mtandao wa kijamii wa WhatsApp jambo lililozua taharuki miongoni mwa watu wengi na kuanza kutaka kujua nini kimemsibu," muungano huo umesema kupitia taarifa.
"Saa 9.09 usiku alituma ujumbe mfupi kwa Mkurugenzi wa Idara ya Sheria TSNP Paul Kisabo ujumbe uliosomeka 'Am at risk!' [Nimo hatarini]."
Muungano huo umesema juhudi za kuwasiliana naye kwa simu kufikia sasa bado hazijafanikiwa.
Wamesema wamepiga ripoti kwa jeshi la polisi katika kituo cha chuo kikuu cha Dar es Salaam.
Taarifa ya chama hicho cha wanafunzi inasema Bw Nondo amekuwa akipokea vitisho kutoka kwa watu wasiojulikana.
Wakati mmoja, anadaiwa kukamatwa na askari wa jeshi la polisi eneo la Milimani City na kutuhumiwa kwamba "analeta uchochezi wa baadhi ya wanafunzi waliokosa mikopo ya elimu ya juu kuandamana."
"Mara kadhaa kumekwua na makundi ya watu asiowatambua na wenye nguo za kiraia wakijitambulisha kama watu wa usalama ambao wamekuwa wakimfuatilia na kumpa vitisho hivyo," taarifa hiyo inasema.
Muungano huo umesema viongozi mbalimbali wa TSNP wamekuwa wakipokea vitisho tofauti tofauti.

Sunday, 4 March 2018

Baraza la Maaskofu Lakomalia Katiba Mpya









Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), limesema ili amani iendelee kuwepo majadiliano ndio nyenzo kuu itakayosaidia kuhuisha mchakato wa Katiba Mpya.

Pia limeitaka Serikali kuweka nia ya dhati na kutii kiu ya Watanzania iwapo wengi wao watahitaji mchakato wa Katiba Mpya uendelezwe.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu wa TEC, Padri Daniel Dulle, wakati akifungua kongamano la kujadili Katiba na ujenzi wa amani wakati wa uchaguzi lililoandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).

Hii ni mara ya pili katika kipindi kisichopungua mwezi mmoja kwa TEC kutoa kauli kama hiyo, kwani kumbukumbu zinaonyesha kuwa Februari 11 mwaka huu, Baraza hilo katika ujumbe wake wa Kwaresma lilitoa msimamo katika masuala matatu kisiasa, kiuchumi na kijamii ambapo lilionya kutozingatia matakwa ya Katiba katika kuendeleza shughuli za kisiasa.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Baraza hilo, Padri Raymond Saba, Padri Dulle, alisema baada ya mchakato wa Katiba Mpya kukwama sasa ni fursa nzuri ya kuendeleza mchakato huo kwa njia ya majadiliano ili kudumisha amani.

“Majadiliano ni nyenzo ya kupambana na tabia ya ubinafsi, ili kujenga umoja huo lazima kuwepo na upendo, mshikamano na maridhiano ya watu na kila mtu kupewa nafasi ya kutoa maoni hata kama yanapingana na mtu mwingine na ukiwa unapatanisha kwa njia hiyo unaitwa mwana wa Mungu.

“Ndilo lengo la kukaa hapa na kujadiliana ili kujenga Taifa letu kwa lengo la kupata Katiba Mpya ambayo kila mmoja anaitamani. Kunapotokea mtafaruku ndipo kunakuwa na chuki kama kikundi kingine hakishirikishwi.  Haki na amani ni matunda tu, kwani ukosefu wa haki ni chanzo cha vita inayoacha makovu na chuki za kisiasa kwenye chaguzi. Kama tunataka kukwepa haya makovu lazima watu tujenge tabia ya kujadiliana,” alisema.

Alisema tangu miaka ya 1800, Kanisa Katoliki limekuwa likitoa miongozo kuhusu masuala ya utawala ili kudumisha amani.

“Suala la Katiba ni nia ya watu wote si ya mtu mmoja, ni sauti ya watu na kadiri watu wanavyohitaji sheria na miongozo. Pengine kikundi kikubwa kinahitaji kidogo hakihitaji cha msingi ni kuangalia wananchi wanahitaji nini kwani kwa mujibu wa ibara ya nane ya Katiba ya sasa, Katiba ni mali ya wananchi,” alisema.

Aidha, akichangia mjadala katika kongamano hilo, Profesa Mwesiga Baregu ambaye alikuwa akimwakilisha Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia nchini (TCD), James Mbatia, alionya Serikali kuhakikisha kabla ya kuingia kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2020, Katiba Mpya inapatikana.

Baregu ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, alisema ni vema kukamilisha kiporo hicho cha Katiba kwa sababu viashiria vyote vya hatari vimekwishaonekana katika chaguzi ndogo zilizofanyika hivi karibuni hususani Jimbo la Kinondoni.

“Tujitahidi kwa vyovyote vile kuhakikisha uchaguzi unaokuja si tu wa haki lakini matokeo yake yawe ya kuaminika. Kwa sababu inaelekea chaguzi zetu kuwa ‘security election’.

“Uchaguzi uliopita Kinondoni tunaambiwa kuna vituo ambavyo polisi walizidi wapiga kura, huu uwapo wa polisi kwenye chaguzi ni tatizo kwa sababu inatafsirika kuwa lazima kutakuwa na machafuko au kuna kitu polisi wamegundua,” alisema.

Aidha, Profesa Baregu, alipendekeza njia tatu za kuendeleza mchakato wa Katiba Mpya kwa kuwa hali iliyopo lazima kuwepo na njia ya kuishawishi Serikali.

“Kwanza twende kwenye kura ya maoni, tunaweza kutangaza kura ya maoni kuhusu Katiba pendekezwa ila sijui kura ya maoni kama itaendeshwa kwa uhuru au haki. Kwa sababu hata katika Katiba pendekezwa tumeona asilimia 85 ya maoni ya wananchi yamenyofolewa.

“Pili kuundwe Bunge la Katiba lenye wajumbe wasiokuwa wabunge kwani hawa waliopo bungeni watatengeneza Katiba ya kuwalinda na tatu kuundwe tume ya wataalamu wa Katiba kama walivyofanya wenzetu Kenya, kwani mahali tulipofika lazima tutoke kwenye ujumla ujumla tuwe na mashinikizo ya kuitaka Serikali ifanye nini kabla ya uchaguzi mkuu ujao,” alisema.

Pamoja na mambo mengine also 

Monday, 26 February 2018

BREAKING NEWS: Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi 'sugu' Kahukumiwa Miezi Mitano Jela


BREAKING NEWS: Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi 'sugu' Kahukumiwa Miezi Mitano Jela




Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya imemuhukumu Miezi Mitano jela Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Michael Mteite ambapo amesema ameridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mteite amesema kuwa Mahakama imejikita katika sehemu kuu nne.

Amesema kuwa sehemu hizo ni kama washtakiwa walitamka Maneno ya fedheha, pia kama maneno waliyoyatoa yamebeba maudhui ya fedheha, pia kama maneno hayo yana mlenga Rais pamoja washtakiwa kama wana hatia ama lah.

Katika hukumu hiyo iliyochukua zaidi ya saa moja Hakimu Mteite amesema amejiridhisha pasina kuacha shaka juu ya ushahidi wa mashahidi watatu wa upande wa mashtaka.

Hakimu Mteite amesema Mahakama inakubaliana na hoja ya kwamba washtakiwa walitamka maneno ya fedheha dhidi ya Rais kutokana na ushahidi wa upande wa mashtaka ambao waliwasikia washtakiwa na kuwaona wakati wakitamka.

“Katika kesi hii mashahidi wengi ni askari, hivyo ni dhahiri wametoa maneno hayo,” -Hakimu Mteite

Pia kuhusu maneno hayo kumlenga Rais Magufuli, Hakimu Mteite amesema maneno hayo ya fedheha ni ya kitaifa, kwani masuala yanayogusa watu kuuawa ni ya kitaifa na ndio maana washtakiwa walitamka maneno (Rais Wetu).

“Tujiulize ni Rais yupi waliyemzungumzia ni wa Simba, Yanga ama Mbeya City hivyo Rais aliyezungumziwa hapa ni Magufuli kwani hakuna Magufuli mwingine anayetuongoza,”-Hakimu Mteite

Hakimu Mteite amesema kwa imani yake washtakiwa wana hatia.

“Kutokana na upande wa utetezi kuomba nafuu ya adhabu na upande wa mashtaka kutaka itolewe adhabu kali, nawahukumu miezi mitano jela,” -Hakimu Mteite.Ed

Saturday, 27 January 2018

Lowassa avaa gwanda kwa Mara ya Kwanza na kumnadi Mgombea wa CHADEMA


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa leo  amepokewa kwa nderemo na wafuasi wa chama hicho.

Lowassa ambaye kwa mara ya kwanza leo Jumamosi Januari 27,2018 amevaa gwanda tangu ajiunge na Chadema mwaka 2015 aliwasili ofisi za chama hicho kanda ya Pwani zilizoko Magomeni, ambako yalianza maandamano kuelekea Mwananyamala ulikofanyika mkutano wa hadhara wa kampeni.

Mkutano huo umefanyika katika uwanja wa Ali Mapilau, Mwananyamala .

Akiongea katika mkutano huo, Lowassa amefunguka na kuwataka wanachama na viongozi wa CHADEMA kuacha kumtaja taja mgombea Ubunge wa CCM Kinondoni Maulid Mtulia kwani mtu huyo ni wa hovyo hastaili kutajwa tajwa kwani kufanya hivyo ni kumpa kichwa.

"Kwanza nawashauri huyu Mtulia msimseme seme sana wanini huyu, mtu hovyo kabisa huyu mnampa kichwa tu sasa mtu hovyo hapaswi kuchukua muda wenu kumjadili bali nachotaka tushughulike kuwaelimisha wananchi wa Kinondoni kwanini wanastahili kutupa sisi kura, habari ya huyu bwana tuachane naye, hawa CCM hawaeleweki kule Moshi na Korogwe tulishinda lakini wakaja kusema tumeshindwa hivyo nataka kusema saizi tujiandae kulinda kura zetu" alisema Lowassa

Mbali na hilo Lowassa alimnadi Salum Mwalimu kwa kusema kuwa ni kijana safi ambaye anastahili kwenda Bungeni kuwasemea wananchi wa Kinondoni

Akizungumzia hatua ya Lowassa kuvaa Gwanda, Katibu wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) Kinondoni, Rose Moshi amesema anadhihirisha kuwa ni kamanda na hakuna sababu ya kuwa na wasiwasi naye.

"Tulikuwa na hofu alipokwenda Ikulu, kuvaa kwake gwanda kunaonyesha kuwa ni mwenzetu," amesema.

Katibu wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam, Jerome Ulomi amesema Lowassa amedhihirisha kuwa ni mwana Chadem

Thursday, 7 December 2017

KISA CHA KUSISIMUA






Nakumbuka enzi hizo nikiwa mtoto mdogo nilikua na tabia ya kuchezea mawe kwa kuyarusha huku na huko.
Siku moja nilirusha jiwe likampata kuku wetu na kufariki palepale. Mama alikuwa akimhusudu sana yule kuku. Kwani alikuwa akitaga mayai mengi sana.
.
Wakati jiwe lilipompata yule kuku na kumuua palepale nilifikiri nilikuwa peke yangu katika mazingira yale. Kumbe dada yangu alikuwa upenuni mwa nyumba yetu akishuhudia jinsi nilivyomuua yule kuku.
.
Hivyo akaniambia, "Deo nimeona ulivyomuua kuku sasa nipe shilingi 50 vinginevyo nitamueleza mama kwamba ni wewe ndiye uliyemuua kuku wake."
.
Nikamwambia "Dada mi kwa sasa sina hiyo hela, tafadhali usimwambie mama, atanichapa kweli"
.
Siku iliyofuata, mama akamwambia dada yangu aoshe vyombo na kufagia uani, ila dada akamwambia mama: "Mama, Deo amesema atafanya usafi na kuosha vyombo yeye."
Halafu akaja kwangu na kuniambia: "Deo, osha vyombo na kufagia uani vinginevyo nitamwambia mama kwamba umemuua kuku wake". Bila kupinga nikaenda kuosha vyombo na kufagia.
.
Siku iliyofuata, mama alimwambia dada yangu aende kuteka maji kisimani na kujaza jaba. Akamwambia mama tena: "Mama, Deo amesema atachota na kujaza peke yake"
.
Hakafu akaja kwangu na kuniambua: "Deo, unamkumbuka yuke kuku uliyemuua? Jaza maji jaba ama sivyo nimueleze mama kwamba wewe ndiye uliyemuua kuku wake..." Hivyo nikajikongoja kuchota maji 'trip' za kutosha mpaka nikajaza jaba.
.
Siku hiyo hiyo jioni nikiwa nimechoka kweli, mama akamtuma dada aende sokoni kununua viazi na mahitaji mengine. Kwa mara nyingine tena akamwambia mama: "Deo amesema anahamu ya kwenda sokoni, anaomba aende yeye kununua."
.
Akaja kangu tena na kunuambia: "Deo, usisahau kuwa kuku bado amekufa, nenda sokoni na ununue viazi na mahitaji haya mengine, vinginevyo...."
Nilichoka!! Nilisimama na kwenda kwa mama huku machozi yakibubujika machoni mwangu, nikamkuta akiwa amekaa akisuka ukiri, nikamfuata na kupiga magoti mikono nimeifumba usawa wa kifua changu huku nikilia nikamwambia;
"Mama, nisamehe mimi. Mimi ndiye niliyemuua kuku wako ila haikuwa makusudi ni bahati mbaya tu katika kucheza kwangu, tafadhali sana mama nisamehe mimi."
.
Mama akanijibu huku akininyanyua: "Mwanangu ile siku umemuua kuku, nilikuwa dirishani nikiangalia kila kilichotokea. Dada yako alikufanya mtumwa wake kwa sababu hukutaka kuja kukiri kosa na kuomba masamaha."
"Lakini kwa kuwa umeona unateseka umekuja kukiri na kuomba msamaha, uko huru sasa, hatakutumikisha tena"

Maana ya yote hayo ni nini?
Kila mara tunavyotenda dhambi, Mungu anatuona na dhambi hizo zinatufanya tuwe watumwa. Kipindi ambacho tutakiri dhambi zetu na kutubu kwa muumba wetu basi atatuweka huru na tutaishi kwa amani, furaha na kheri.
Basi Mwenyezi Mungu atujalie tuwe na moyo wa toba ya kweli pale tunapokengeuka...Amen!
Comment na SHARE