Tuesday, 7 June 2016

Pele kupiga mnada medali zake zote


Mshirikishe mwenzako
Image copyrightACTION PLUS SPORTS IMAGES ALAMY STOCK PHOTO
Image captionPele kupiga mnada medali zake zote
Nyota wa soka kutoka Brazil, Pele, ameamua kupiga mnada medali zote alizoshinda na vitu vingine vyenye dhamani alivyopata wakati alipokuwa mchezaji nguli duniani .
Image copyrightDIVULGACAO I HALCYON GALLERY
Image captionMnada huo utakaodumu muda wa siku tatu, unaanza leo mjini London
Mnada huo utakaodumu muda wa siku tatu, unaanza leo mjini London na unatarajiwa kukusanya mamilioni ya pesa.
Image copyrightJULIENS
Image captionBaadhi ya medali za Pele zitakazouzwa leo mjini London
Wataalamu wanasema huenda mnada huo ukawa ndio mkubwa zaidi wa vifaa vya michezo kuwahi kufanyika.
Image captionMedali zote alizoshinda wakati wa kombe la dunia pia zitauzwa
Medali zote alizoshinda wakati wa kombe la dunia pia zitauzwa wakati wa mnada huo.
Image copyrightJULIENS
Image captionViatu alivyochezea katika kombe la dunia
Nyota huyo wa zamani amesema atatoa sehemu ya fedha zitakazo patikana kwa mashirika ya kutoa misaada na kuongeza kwamba angelipenda historia yake kufurahiwa na kuonyesha katika makaazi ya watu na makavazi kote duniani.
Image copyrightGETTY
Image captionPele ambaye alianza kuchezea Brazil mika 60 iliyopita anasalia kuwa mfungaji bora zaidi wa mabao nchini humo.
Pele ambaye alianza kuchezea Brazil mika 60 iliyopita anasalia kuwa mfungaji bora zaidi wa mabao nchini humo

No comments: