Thursday, 4 August 2016

FUATILIA HIKI KISA

Tahadhari Kwa Wakenya : Uchawi Ni Utumwa.


                             Na. THEOFLIDA  WA  YESU.
Naanza  kwa  kuwasalimu  kwa  JINA  LA  YESU. Jina  lililo  Kuu  kupita  majina  yote. 
 
Wiki  kadhaa  zilizo  pita, niliandika  waraka  wangu   kwa  watanzania  na  kuusambaza   kupitia  blogs  na  mitandao  mbalimbali   kuhusu  athari  za  kujihusisha  na  masuala  ya  waganga  wa  jadi  . 

Katika waraka  huo   niliwatahadharisha  watanzania  kutojihusisha  na  WAGANGA  WA  TUNGULI  kwa  sababu WAGANGA  WA  TUNGULI  ni   WACHAWI NA MAWAKALA  WA  SHETANI   walio  vaa  kofia  ya  utabibu.

KUUSOMA  WARAKA  HUO, TAFADHALI  TEMBELEA 

:http://shuhudazaajabu.blogspot.co.ke/2016/07/ushuhuda-nilimlisha-mume-wa-mtu.html
 
  AU
 http://www.mpekuzihuru.com/2016/07/ushuhuda-nilimlisha-mume-wa-mtu.html
 
Katika  waraka  huo  niliwaelezea  watanzania  jinsi  nilivyo  shawishika  kutafuta  msaada  wa  maisha  yangu   kwa  MGANGA  WA  TUNGULI  aitwae  MUNGU  WA  KABILI  na  kujikuta  nikipata  matatizo  makubwa  ambayo  hata  hivyo  yalipelekea  kunikutanisha  na  YESU  ambae  ameniokoa.

Katika  waraka  huo nili  sahau  kueleza  mambo  makuu  mawili yafuatayo:

Kwanza  nilisahau  kuweka  mawasiliano  ya   MUNGU  WA  KABILI   ayatumiayo pindi  anapokuwa  nchini  KENYA ili  kuwa  tahadharisha  wakenya  wasipige  namba  hiyo  wala  wasijaribu  kutafuta  msaada  kwenye  namba  hiyo, kwa  sababu  mtu  huyo  ni  WAKALA  WA  SHETANI  alie  jificha  kwenye  kivuli  cha  UGANGA...

Wengi  walio  jaribu  kutafuta  msaada  kwa  MUNGU  WA  KABILI  wamejikuta  wakiishia  kuunganishwa  na  UTAWALA  WA  KUZIMU  ambao  umewapelekea  kujikuta  katika  matatizo  makubwa  kama   niliyo  yapata  mimi.

Nimeona  vyema  kuwatahadharisha  wakenya, kwa  sababu  mungu  wa  kabili  hufanya  kazi  zake  Tanzania  na  Kenya.  Anapokuwa  Tanzania, namba  yake  huwa  ni  + 255  744  000  473  na  anapokuwa  Kenya , namba  yake  huwa  ni  + 254    704  71 61 59.
 
Hivyo  basi   Ndugu  zangu Wakenya , hii ni  tahadhari  yangu  kwenu. Nimeweka  namba  hizo  hapo  juu  kama  alama  ya  MPINGA  KRISTO  ambayo  watu  wote  wenye  hofu  ya  Mungu  wanapaswa  kuepukana  nayo..

Nimeongozwa  katika  namna  ya  rohoni, kuanza  kufanya  kampeni  ya  nguvu  dhidi  ya  roho  ya  kuhusudu  masuala  ya  UGANGA, UCHAWI  NA  USHIRIKINA  na  nitajikita  zaidi  katika  mapambano  dhidi  ya  MGANGA  WA  JADI  AITWAE  MUNGU  WA  KABILI.
 
Ninaanza  kwa  kupambana  na  MUNGU  WA  KABILI  kwa  sababu, kwa  miaka  zaidi  ya  mitatu  ambayo  nimekuwa  nikishirikiana  na  MUNGU  WA  KABILI,  nimeweza  kujua  kuwa  yeye    ndio   MKUU  WA  WAGANGA  NA  WACHAWI  WOTE  WA  AFRIKA  MASHARIKI  NA  KATI , na  watu  wenye  hekima  wanasema  katikati  ya  kundi  la  kondoo  MPIGE  RUNGU  MCHUNGAJI, NA  KONDOO  WOTE  WATATAWANYIKA.

Naamini  nikimsambaratisha  mungu  wa  kabili, basi itakuwa  rahisi  kwa  waganga  wengine  kwa  sababu  wote  ni  kama  wafuasi  wake  tu.

Katika  kampeni  yangu  hii  ya  kiroho, nimeanzisha  blogu  iitwayo  SHUHUDA  ZA  AJABU  ambayo  inapatikana : www.shuhudazaajabu.blogspot.com.
 
Nitakuwa  nikitoa  shuhuda  za  mambo  mbalimbali  ya  kichawi  niliyo fundishwa  na  MUNGU  WA  KABILI  na  jinsi  unavyo  weza  kujiepusha  nayo  kwa  kutumia  Jina  la  Yesu.

Najua  kazi  hii  itainua  uadui  mkubwa  dhidi  yangu, kwa  sababu  hakuna  kitu  wachawi  wanakichukia  kama siri  zao  kutolewa  hadharani, lakini  kwa  Jina  la  Yesu, nitapambana  vita  hii  na  nitaishinda.
 
 MUNGU  WA  KABILI  na  jeshi  lake  watajaribu  kushindana  na  mimi  lakini  hawatashinda.( YEREMIA 1:19.)
 
Shuhuda  nitakazo  zitoa, zitakuwa  na  mafundisho  mazuri yatakayo  kupa  faida  , kama  Mungu  anavyo  sema katika  kitabu  cha ISAYA  48  kwamba  " MIMI  NI  MUNGU  NIKUFUNDISHAE  ILI  UPATE  FAIDA'.

Ushuhuda  huu  utakufanya  umjue  shetani  vizuri kama  wasemavyo  watu  wenye  hekima  " MJUE  ADUI  YAKO  KAMA  UNAVYO   IJUA  NAFSI  YAKO"

JAMBO  LA  PILI  na  la  msingi  ambalo  sikuweza  kuli

No comments: