Saturday, 29 July 2017

Korea Kaskazini yafanyia majaribio kombora jingine


Kombora lililorushwa na Korea Kaskazini
Image captionKombora lililorushwa na Korea Kaskazini
Korea Kaskazini imefanya jaribio jingine la kombora, kulingana na maafisa wa Japan na Korea kusini.
Kombora hilo limeonekana likianguka katika bahari ya Japan kulingana na chombo cha habari cha kitaifa cha Japan.
Mapema mwezi Julai, Pyongyang ilidai kufanikiwa kulifanyia majaribio kombora la masafa marefu kwa mara ya kwanza.
Kombora hilo ni la hivi karibuni katika msururu wa makombora yaliofanyiwa majaribio hatua inayokiuka marufuku ya UN.
Umbali wa kombora hilo haujulikani.
Umbali wake umepingwa lakini wataalam wanasema kuwa linaweza kufika Alaska nchini Marekani.
Msemaji wa Pentagon Jeff Davis alisema kuwa kombora hilo lilirushwa na kwamba habari zaidi zinasubiriwa.
Kombora hilo la hivi karibuni ni la 14 kurushwa na Korea Kaskazini 2017.
Kombora hilo lilirushwa kutoka mkoa wa Jagang kaskazini mwa taifa hilo , kulingana na chombo cha habari cha Korea kusini Yonhap.
Katibu wa baraza la mawaziri nchini Japan Yoshihide Suga alisema kuwa kombora hilo lilisafiri kwa takriban dakika 45 ikilinganishwa na kombora la masafa marefu lililofanyiwa majaribio mapema mwezi Julai.
Anasema kuwa lilianguka katika bahari ya Japan, lakini sio katika maji ya himaya ya Japan.
Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in ameitisha mkutano wa kiusalama katikati ya usiku kulingana na Yonhap

Tuesday, 30 May 2017

ANZA NA BWANA, YOTE YAWEZEKANA KWAKE YEYE AAMINIE




“Walipowafikia wale wanafunzi wengine, wakawakuta wamezungukwa na umati mkubwa wa watu na baadhi ya walimu wa sheria wakibishana nao. Mara wale watu walipomwona Yesu, wakastaajabu sana, wakamkimbilia, ili kumsalimu.
Akawauliza wanafunzi Wake, “Mnabishana nao kuhusu nini?’’
Mtu mmoja miongoni mwa ule umati wa watu akajibu, “Mwalimu, nilimleta kwako mwanangu ambaye ana pepo mchafu ambaye ana mfanya asiweze kuongea. Kila mara huyo pepo mchafu ampagaapo mwanangu, humwangusha chini na kumfanya atokwe povu mdomoni na kusaga meno, kisha mwili wake hukauka. Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo mchafu, lakini hawakuweza.’’
Yesu akawaambia, “Enyi kizazi kisicho na imani! Nitakuwa pamoja nanyi mpaka lini? Nitachukuliana nanyi mpaka lini? Mleteni huyo mvulana kwangu.”
Nao wakamleta yule mvulana. Yule pepo mchafu alipomwona Yesu, mara akamtia yule mvulana kifafa, akaanguka, akagaagaa chini huku akitokwa na povu kinywani.
Yesu akamwuliza baba yake, “Mwanao amekuwa akitokewa na hali hii tangu lini?’’ Akamjibu, “Tangu utoto wake. Mara kwa mara huyo pepo mchafu amekuwa akimwangusha kwenye moto au kwenye maji ili kumwangamiza. Lakini kama unaweza kufanya jambo lo lote, tafadhali tuhurumie utusaidie.’’

Yesu akamwambia, “Kama ukiweza kuamini, yote yawezekana kwake yeye aaminiye.’’ Mara baba yake yule mvulana akapiga kelele akisema, “Ninaamini. Nisaidie kutokuamini kwangu!’’ Yesu alipoona kwamba umati wa watu unakusanyika pamoja mbio, akamkemea yule pepo mchafu, akimwambia, ‘‘Wewe pepo bubu na kiziwi, nakuamuru umtoke wala usimwingie tena!”
Yule pepo mchafu akiisha kupiga kelele, akamtia kifafa kwa nguvu, akamtoka. Yule mvulana alikuwa kama maiti, hivyo watu wengi wakasema, ‘‘Amekufa.’’ Lakini Yesu akamshika mkono akamwinua, naye akasimama.
Baada ya Yesu kuingia ndani ya nyumba, wanafunzi Wake wakamwuliza wakiwa peke yao, ‘‘Mbona sisi hatukuweza kumtoa huyo pepo mchafu?’’
Yesu akawajibu, ‘‘Hali hii haiwezi kutoka isipokuwa kwa kuomba na kufunga’’ #MARKO 9:14-29

Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo aliye hai ewe mpendwa wangu.

Mwana wa Mungu kwanza napenda kumshukuru Mungu ambaye anaendelea kututia nguvu katika kazi yake. Nakushukuru wewe ambaye huchoki kuomba kwa ajili yetu kama nasi pia tusivyochoka kuomba kwa ajili yenu. Mungu aliye hai na mwaminifu anajua namna gani tunakesha kwa ajili yenu. Ainuliwe Mungu ambaye haachi kutuhuisha hata pale tunapokuwa tumechoka. Nami ni maombi yangu Roho wa Kristo akuhuishe roho na nafsi yako unapokuwa umechoka. Imeandikwa ‘Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume kujikwaa na kuanguka, bali wale wamtumainio BWANA atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai, watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia. #Isaya 40:30-31

Ni maombi yetu Mungu afanye upya nguvu zako za rohoni upae juu kama tai usirudi nyuma katika jina la Yesu.

Mpendwa wangu Bwana Yesu anatuambia siri ya ajabu sana hapa kuhusu Imani na kufunga na kuomba. Kwenye #WARUMI 15:4 imeandikwa ‘kila kitu kilichoandikwa zamani, kiliandikwa kutufundisha, ili kwamba kwa saburi na faraja tunayopata katika Maandiko tuwe na tumaini’. Jambo hili lililowatokea wanafunzi wa Yesu kushindwa kumtoa pepo ndani ya kijana yule aliyekuwa kwenye mateso makubwa ni mfano mzuri tu kwa kanisa la leo. Kwani ni mambo mangapi tumefeli kuyatatua kwenye kanisa? Watu wangapi wamekuja wakisumbuliwa na nguvu za pepo wachafu halafu wanaondoka bila msaada. Ushawahi kujiuliza kwanini watumishi Fulani waweze kuwasaidia watu kufunguliwa toka kwenye mateso lakini sio wewe au sio ninyi kanisani kwenu?

Mahali Fulani nilikuta kanisa moja Mchungaji amechukua mke wake kwenda kuombewa sehemu Fulani kwa kuwa yeye na kanisa lake hawaamini katika uponyaji na miujiza ya Yesu! Yamkini sisi sote kwa namna moja au nyingine tumepitia katika kufeli kushindwa kuwasaidia watu wenye shida za namna mbalimbali kwa sababu hatuamini katika uponyaji wa Yesu au hatuna nguvu za rohoni kufanya hivyo. Lakini hilo

Saturday, 20 May 2017

BASKETBALL GAME YA KUKATA NA SHOKA ,MADAKTARI SFUCHAS VS MOROGORO WORRIORS 21/MAY/2017 JUMAPILI




Kutakuwepo na mchezo wa basketball kati ya SFUCHAS na MOROGORO WORRIORS katika viwanja vya jkt hapa morogoro mjini mchezo utakaofanyika kesho jumapili kuanzia mida ya saa kumi jion.Mchezo huo utakuwa na ushindani mkubwa haijapata kutokea kutokana na umahiri wa timu hizi mbili.SFUCHAS  watakuwa wageni Katika huo mchezo wakiongozwa na captain wao GIDEON akisaidiwa na ndugu MAZIKU .Sambamba na hilo mnaombwa wanafunzi wate kwa umoja wenu kuhudhuria mpambano huo wa kukata na shoka bila kukosa mkiwa kauli mbiu ya SFUCHAS USHINDI LAZIMA.
Ni baadhi ya picha za kikosi cha timu ya Sfuchas .