Thursday, 7 December 2017

KISA CHA KUSISIMUA






Nakumbuka enzi hizo nikiwa mtoto mdogo nilikua na tabia ya kuchezea mawe kwa kuyarusha huku na huko.
Siku moja nilirusha jiwe likampata kuku wetu na kufariki palepale. Mama alikuwa akimhusudu sana yule kuku. Kwani alikuwa akitaga mayai mengi sana.
.
Wakati jiwe lilipompata yule kuku na kumuua palepale nilifikiri nilikuwa peke yangu katika mazingira yale. Kumbe dada yangu alikuwa upenuni mwa nyumba yetu akishuhudia jinsi nilivyomuua yule kuku.
.
Hivyo akaniambia, "Deo nimeona ulivyomuua kuku sasa nipe shilingi 50 vinginevyo nitamueleza mama kwamba ni wewe ndiye uliyemuua kuku wake."
.
Nikamwambia "Dada mi kwa sasa sina hiyo hela, tafadhali usimwambie mama, atanichapa kweli"
.
Siku iliyofuata, mama akamwambia dada yangu aoshe vyombo na kufagia uani, ila dada akamwambia mama: "Mama, Deo amesema atafanya usafi na kuosha vyombo yeye."
Halafu akaja kwangu na kuniambia: "Deo, osha vyombo na kufagia uani vinginevyo nitamwambia mama kwamba umemuua kuku wake". Bila kupinga nikaenda kuosha vyombo na kufagia.
.
Siku iliyofuata, mama alimwambia dada yangu aende kuteka maji kisimani na kujaza jaba. Akamwambia mama tena: "Mama, Deo amesema atachota na kujaza peke yake"
.
Hakafu akaja kwangu na kuniambua: "Deo, unamkumbuka yuke kuku uliyemuua? Jaza maji jaba ama sivyo nimueleze mama kwamba wewe ndiye uliyemuua kuku wake..." Hivyo nikajikongoja kuchota maji 'trip' za kutosha mpaka nikajaza jaba.
.
Siku hiyo hiyo jioni nikiwa nimechoka kweli, mama akamtuma dada aende sokoni kununua viazi na mahitaji mengine. Kwa mara nyingine tena akamwambia mama: "Deo amesema anahamu ya kwenda sokoni, anaomba aende yeye kununua."
.
Akaja kangu tena na kunuambia: "Deo, usisahau kuwa kuku bado amekufa, nenda sokoni na ununue viazi na mahitaji haya mengine, vinginevyo...."
Nilichoka!! Nilisimama na kwenda kwa mama huku machozi yakibubujika machoni mwangu, nikamkuta akiwa amekaa akisuka ukiri, nikamfuata na kupiga magoti mikono nimeifumba usawa wa kifua changu huku nikilia nikamwambia;
"Mama, nisamehe mimi. Mimi ndiye niliyemuua kuku wako ila haikuwa makusudi ni bahati mbaya tu katika kucheza kwangu, tafadhali sana mama nisamehe mimi."
.
Mama akanijibu huku akininyanyua: "Mwanangu ile siku umemuua kuku, nilikuwa dirishani nikiangalia kila kilichotokea. Dada yako alikufanya mtumwa wake kwa sababu hukutaka kuja kukiri kosa na kuomba masamaha."
"Lakini kwa kuwa umeona unateseka umekuja kukiri na kuomba msamaha, uko huru sasa, hatakutumikisha tena"

Maana ya yote hayo ni nini?
Kila mara tunavyotenda dhambi, Mungu anatuona na dhambi hizo zinatufanya tuwe watumwa. Kipindi ambacho tutakiri dhambi zetu na kutubu kwa muumba wetu basi atatuweka huru na tutaishi kwa amani, furaha na kheri.
Basi Mwenyezi Mungu atujalie tuwe na moyo wa toba ya kweli pale tunapokengeuka...Amen!
Comment na SHARE

Monday, 30 October 2017

BREAKING NEWS MBUNGE WA SINGIDA KASKAZINI RAZARO NYARANDU AJIUZURU NA KUOMBA KUHAMIA CHADEMA.













NIMEAMUA kujiuzulu NAFASI yangu ya Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM, pamoja na nafasi zote za Uongozi ndani ya Chama kuanzia leo, Oktoba 30, 2017. HALIKADHALIKA, asubuhi ya leo nimemwandikia Spika wa Bunge, Mh. Job Ndugai, Mb., barua ya kujiuzulu nafasi yangu ya UBUNGE wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia tiketi ya CCM, nafasi ambayo nimeitumikia kwa vipindi vinne mfululizo tangu nilipochaguliwa kwa mara ya kwanza mnamo mwaka 2000 hadi Sasa.

AIDHA, Nimechukua UAMZI huo kutokana na kutorishwa kwangu na mwenendo wa hali ya Kisiasa nchini, ikiwa ni pamoja na ukiukwaji wa HAKI za Kibinadamu, ongezeko la vitendo vya dhuluma wanavyofanyiwa baadhi ya watanzania wenzetu, na kutokuwepo kwa mipaka ya wazi kati ya MIHIMILI ya dola (Serikali, Bunge, na Mahakama) kunakofanya utendaji kazi wa Kibunge wa Kutunga Sheria na wa Kuisimamia Serikali kutokuwa na uhuru uliainishwa na kuwekwa bayana KIKATIBA.

VILEVILE, Naamini kwamba bila Tanzania kupata Katiba Mpya Sasa, hakuna namna yeyote ya kuifanya mihimili ya dola isiingiliane na kuwepo kwa ukomo wa wazi na kujitegemea kwa dhahiri kwa mihimili ya Serikali, Bunge na mahakama ambayo ndio chimbuko la Uongozi Bora wa nchi, na kuonesha kwa uwazi kuwa madaraka yote yatokana na wananchi wenyewe, na kwamba Serikali ni ya Watu kwajili ya Watu.

MIMI Naondoka na kukiacha Chama Cha Mapinduzi CCM, nikiwa nimekitumikia kuanzia ngazi ya Uenyekiti wa UVCCM Mkoa, Ujumbe wa Kamati za Siasa Wilaya na Mkoa, Ujumbe wa Kamati ya Wabunge Wote wa CCM na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM TAIFA, kwani nimejiridhisha kuwa kwa mwenendo wa hali ya kisiasa, kiuongozi na kiuchumi uliyopo Tanzania Sasa, CCM imepoteza mwelekeo wake wa kuisimamia Serikali kama ilivyokuwa hapo awali. AIDHA, Naamini kuwa, kama ilivyotokea kwa mihimili ya Bunge na Mahakama kutokuwa na uhuru kamili, bila kuingiliwa kiutendaji kwa namna Moja au nyigine, CCM nayo imekuwa Chini ya miguu ya dola badala ya chama kushika hatamu na kuikosoa Serikali inapobidi kama yalivyokuwa maono ya Baba wa TAIFA MWALIMU Julius Kambarage Nyerere.

HIVYOBASI, kwa dhamira yangu, na kwa uamuzi wangu mwenyewe, nikiwa na haki ya KIKATIBA, natangaza KUKIHAMA Chama Cha Mapinduzi CCM


HISTORIA YAKE:

Lazaro Nyalandu alizaliwa Agosti 18, 1970 mkoani Singida.

Nyalandu alipata elimu ya msingi katika shule za Pohama na Mrumba zilizoko kijijini kwao huko mkoani Singida na kuhitimu mwaka 1987. Aliendelea na masomo ya kidato cha kwanza mpaka cha nne katika Shule ya Sekondari Kibaha mkoani Pwani (1988 – 1991) na alifaulu vizuri na kujiunga na Shule ya Sekondari Ilboru ambako alisoma kidato cha tano na sita.

Wakati akiwa mwanafunzi wa sekondari, Nyalandu alikuwa kiongozi wa juu wa Ushirika wa Kikristo wa Wanafunzi Tanzania (Ukwata) 1991 – 1993 na baadaye alikuwa miongoni mwa vijana wa Kitanzania walioteuliwa kuzuru jiji la Rio De Janeiro, Brazil na kushuhudia mkutano wa Mazingira mwaka 1993.

Nyalandu alipata elimu yake ya Chuo Kikuu nchini Marekani ambako alihitimu Shahada ya kwanza ya Sanaa katika Usimamizi wa Biashara (BBA) mwaka 1997 katika Chuo Kikuu cha Wartburg.

Kabla ya hapo alikuwa amepata Shahada ya Biashara ya Kimataifa kutoka Chuo Kikuu cha Wardorf nchini humo. Kiongozi huyu, sasa ana Shahada ya Uzamili aliyoipata kwa njia ya utafiti kutoka Chuo Kikuu cha Buckingham, Uingereza akifuzu katika masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa na Diplomasia.

Baada ya kuhitimu masomo yake ughaibuni, Nyalandu alianza kazi huko huko Marekani katika Benki ya North West, akifanya kazi katika kitengo cha operesheni za kibenki kati ya mwaka 1998–1999.

Aliporejea nchini Tanzania alifanikiwa kuwa sehemu ya washauri wa mke wa aliyekuwa Rais Benjamin Mkapa, Mama Anna Mkapa, katika uendeshaji wa taasisi ya Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF).

Ushauri wa timu yake ulisaidia taasisi hiyo kupata misaada mingi kutoka nchi za Ulaya, Marekani, China na nyinginezo. Pia, alikuwa anamsaidia mama huyo katika uandishi wa hotuba zake pale alipokuwa na majukumu makubwa ya kitaifa na k
I

Sunday, 17 September 2017

BREAKING NEWS *NACTE ; MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KATIKA VYUO VYA AFYA NA UALIMU VYA SERIKALI 2017/18


BREAKING NEWS *NACTE ; MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KATIKA VYUO VYA AFYA NA UALIMU VYA SERIKALI 2017/18* NACTE Imetangaza kumalizika kwa Uhakiki wa Udahili wa Wanafunzi wanaotarajia kujiunga kwenye vyuo vya Serikali, Afya na Ualimu , Unaweza kuangalia matokeo ya Selection kwa kubofya kwenye linki hapo👇👉👉http://www.tzjobconnection.com/2017/09/nacte-diploma-and-certificate-selection.html

*http://www.tzjobconnection.com/2017/09/nacte-diploma-and-certificate-selection.html