UN yaitupia lawama Boko Haram
Mshirikishe mwenzako
Umoja wa Mataifa umelilaumu kundi la itikadi kali la Boko Haram kwa ghasia ambazo imeziita zisizoeleweka na ukatili nchini Nigeria
Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja huo Stephen O'brien amesema hatua za kundi hilo zimefanya idadi kubwa ya watu kuyakimbia makaazi yao.
Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa zaidi ya watu milioni tisa wamevuka bonde la mto Chad na kuelekea maeneo mengine ya Nigeria, Niger, Chad na Cameroon kwa lengo la kutafuta msaada wa kibinadamu
No comments:
Post a Comment