Wednesday, 24 August 2016

Ndege ndefu zaidi duniani yapata ajali



AirlanderImage copyrightSBNA
Image captionNdege hiyo imeharibika sehemu wanamoketi marubani



AirlanderImage copyrightSBNA
Image captionAirlander 10 ilikuwa inarejea uwanja wa ndege wa Cardington Airfield
Kampuni ya HAV inapanga kuunda ndege 10 aina ya Airlander kufikia mwaka 2021.
Airlander 10Image copyrightSBNA
Image captionHAV inapanga kuunda ndege 10 za Airlander kufikia mwaka 2021

Airlander 10 kwa takwimu
  • 44,100 lbs (20,000kg): Uzani wa ndege hiyo
  • 20,000ft (6,100m): Umbali ambao inaweza kupaa juu angani
  • 80 knots (148km/h): Kasi yake ya juu zaidi
  • Siku 5: Muda ambao inaweza kukaa angani
  • 22,050 lbs (10,000kg): Uzani ambao inaweza kubeba

AirlanderImage copyrightSOUTH BEDS NEWS AGENCY
Image captionNdege hiyo imeharibika eneo wanamoketi marubani

Ndege ndefu zaidi duniani - Airlander 10 - imeharibika baada ya kuanguka ikitua kwenye safari yake ya pili ya kufanyiwa majaribio.
Ndege hiyo ya urefu wa 302ft (92m) - ambayo kwa kiasi fulani ni ndege na pia kwa kiasi fulani puto - iliharibika ikiwa katika uwanja wa Cardington, Bedfordshire nchini Uingereza.
Ndege hiyo ya thamani ya £25m imeharibika eneo wanamoketi marubani baada ya kuangika kwa 'pua' mwendo wa saa tano saa za Uingereza.
Msemaji wa HAV, kampuni iliyounda ndege hiyo, amesema marubani na wahudumu wengine wote wako salama.
Kampuni hiyo imekanusha madai kwamba waya uliokuwa umening'inia kutoka kwenye ndege hiyo ulikwama kwenye kigingi cha nyaya za simu na kusababisha ajali hiyo.
Ndege hiyo ilifanya safari yake ya kwanza 17 Agosti.
AirlanderImage copyrightSBNA
Image captionNdege hiyo imeharibika sehemu wanamoketi marubani
AirlanderImage copyrightSBNA
Image captionAirlander 10 ilikuwa inarejea uwanja wa ndege wa Cardington Airfield
Kampuni ya HAV inapanga kuunda ndege 10 aina ya Airlander kufikia mwaka 2021.
Airlander 10Image copyrightSBNA
Image captionHAV inapanga kuunda ndege 10 za Airlander kufikia mwaka 2021

Airlander 10 kwa takwimu
  • 44,100 lbs (20,000kg): Uzani wa ndege hiyo
  • 20,000ft (6,100m): Umbali ambao inaweza kupaa juu angani
  • 80 knots (148km/h): Kasi yake ya juu zaidi
  • Siku 5: Muda ambao inaweza kukaa angani
  • 22,050 lbs (10,000kg): Uzani ambao inaweza kubeba

AirlanderImage copyrightSOUTH BEDS NEWS AGENCY
Image captionNdege hiyo imeharibika eneo wanamoketi marubani




Ndege ndefu zaidi duniani - Airlander 10 - imeharibika baada ya kuanguka ikitua kwenye safari yake ya pili ya kufanyiwa majaribio.
Ndege hiyo ya urefu wa 302ft (92m) - ambayo kwa kiasi fulani ni ndege na pia kwa kiasi fulani puto - iliharibika ikiwa katika uwanja wa Cardington, Bedfordshire nchini Uingereza.
Ndege hiyo ya thamani ya £25m imeharibika eneo wanamoketi marubani baada ya kuangika kwa 'pua' mwendo wa saa tano saa za Uingereza.
Msemaji wa HAV, kampuni iliyounda ndege hiyo, amesema marubani na wahudumu wengine wote wako salama.
Kampuni hiyo imekanusha madai kwamba waya uliokuwa umening'inia kutoka kwenye ndege hiyo ulikwama kwenye kigingi cha nyaya za simu na kusababisha ajali hiyo.
Ndege hiyo ilifanya safari yake ya kwanza 17 Agosti.
AirlanderImage copyrightSBNA
Image captionNdege hiyo imeharibika sehemu wanamoketi marubani
AirlanderImage copyrightSBNA
Image captionAirlander 10 ilikuwa inarejea uwanja wa ndege wa Cardington Airfield
Kampuni ya HAV inapanga kuunda ndege 10 aina ya Airlander kufikia mwaka 2021.
Airlander 10Image copyrightSBNA
Image captionHAV inapanga kuunda ndege 10 za Airlander kufikia mwaka 2021

Airlander 10 kwa takwimu
  • 44,100 lbs (20,000kg): Uzani wa ndege hiyo
  • 20,000ft (6,100m): Umbali ambao inaweza kupaa juu angani
  • 80 knots (148km/h): Kasi yake ya juu zaidi
  • Siku 5: Muda ambao inaweza kukaa angani
  • 22,050 lbs (10,000kg): Uzani ambao inaweza kubeba

AirlanderImage copyrightSOUTH BEDS NEWS AGENCY
Image captionNdege hiyo imeharibika eneo wanamoketi marubani

Jeshi La Polisi Lahusisha Mauaji ya Polisi Wanne na Sakata la Oparesheni UKUTA.........Lapiga Marufuku Mikutano yote ya Ndani ya Vyama vya Siasa


KUFUATIA mauaji ya askari wanne yaliyotokea Kata ya Mbande Temeke kwa watu wanaodhaniwa ni majambazi kuvamia benki ya CRDB na kuwaua askari hao kwa kutumia silaha za moto jeshi la Polisi limetangaza kiama na kuwataka wahusika wote kujisalimisha.

Katika hatua nyingine jeshi la polisi limehusisha tukio hilo na Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (UKUTA) kufuatia matamko ya baadhi ya viongozi wa kisiasa ambao wamesikika katika majukwaa ya kisiasa wakihamasisha wafuasi wao wawashambulie askari wa Jeshi la Polisi.

Kauli hiyo imetolewa  na Kamishna Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Nsato Marijan Mssanzya (CP), wakati akizungumza waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana ambapo pia alikiri kuwa mazoezi yanayofanywa na polisi yamelenga kukabiliana na Ukuta.

Akizungumza kwa hisia CP Mssanzya pia amepiga marufuku  mikutano ya ndani yenye viashiria vya uchochezi na hata ikifanyika kwenye majukwaa watamshusha muhusika na kumfikisha kwenye mkono wa sheria.

Amesema Jeshi  hilo limebaini kwamba mikutano hiyo imekuwa ikitumika kuchochea wananchi na kuwahamasisha kuvunja sheria za nchi na kufanya mapambano na jeshi la polisi

"Kwasababu hiyo basi,kwa hali ya kutumia mikutano ya ndani kuchochea watu kuvunja sheria na kupambana na askari, hivyo basi kuanzia sasa jeshi la polisi nchini linapiga marufuku mikutano yote ya ndaniamesema.
Aidha CP  Mssanzya  aliwataja askari waliouawa katika tukio hilo wakati wakibadilishana lindo kuwa ni  E.5761 CPL Yahya, F.4660 CPL Hatibu, G 9524 PC Tito na G 9996 PC Gastoni na raia wawili waliojeruhiwa aliowataja kuwa Ali Chiponda na Azizi Yahya wote wakiwa wakazi wa Mbande.

"Katika tukio hilo majambazi ambao idadi yao haikufahamika walifanikiwa kupora silaha mbili aina ya MSG na lisasi 60 na hakuna pesa wala mali ya benki hiyo kuibiwa au kuharibiwa, ni dhahiri kuwa waharifu hao walikuwa na kusudio moja tu la kuwashambiulia askari polisi, " alisema.

Alisema katika hali ya kushangaza baada ya tukio hilo kuna baadhi ya watu waliandika mitandaoni kubeza na kukeji mazoezi ya kawaida ya jeshi la polisi na wengine waliandika ujembe wa kushabikia tukio hilo la kuuawa kwa askari polisi huku wengine wakidiriki kuandika ujumbe unaosema endapo watapigwa na polisi Septemba1 mwaka huu basi viongozi wa jeshi hilo wawaondoe askari wanaoishi uraiani na kuwarudisha kambini.

Aliongeza kuwa jeshi la polisi limejipanga vyema kukabiliana na matukio yote ya uvunjifu wa amani nchini.
Waandishi wa habari wakichukua taarifa hiyo.

Monday, 22 August 2016

Lowassa, Mbowe na Katibu Mkuu Chadema Waanza Mikakati ya UKUTA





Siku moja baada ya Chadema kutangaza safu ya Ukuta, viongozi wa chama hicho wameanza kutawanyika mikoani kuanza kutoa elimu ya mpango huo.

Wakati mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe akiwa Kanda ya Kaskazini aliyekuwa mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa alikuwa mkoani Mbeya na jana alishiriki ibada na kuanza vikao vya mkakati huo.

Mbowe jana alikutana na viongozi wa kanda hiyo na kuunda kamati zitakazokwenda katika majimbo yote 35 ya uchaguzi katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara kutoa elimu.

Mbowe alisema katika kikao hicho, ambacho ni mfululizo wa vikao vinavyoendelea kanda zote nchini, wamekubaliana kutoa elimu ya dhana ya Ukuta.

Hata hivyo, alisema bado chama hicho kimetoa fursa ya mazungumzo kwa taasisi yoyote ili kuhakikisha mgogoro uliosababisha Kamati Kuu kuunda Ukuta.

Wakati Mbowe akisema hayo, Lowassa ametua katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini inayojulikana kama Kanda ya Nyasa akiwa na mambo matatu makubwa.

Aliwasili jana asubuhi kwa ndege ma kwenda moja kwa moja kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Forest akiwa na viongozi wa chama hicho wa kanda pamoja na wabunge mbalimbali wa majimbo ya mikoa ya Mbeya, Njombe, Iringa, Songwe, Rukwa na wale wa viti maalumu.

Waziri Mkuu huyo wa zamani, alishiriki ibada ya kawaida na alipokea zawadi ya nyimbo zilizowekwa kwenye ‘flash’ kutoka kwa wanakwaya wa kanisa hilo huku naye akiwachangia kwa kuendesha harambee ya papo kwa papo kutoka kwa viongozi alioongozana nao.

Katika harambee hiyo, zilipatikana Sh4 milioni zikiwamo Sh 1 milioni ambazo aliahidi kuzitoa.

Kabla ya ibada kumalizika, Lowassa na ujumbe wake waliondoka kwenda kwenye kikao cha Baraza la Chadema la Kanda.

Katibu wa Kanda hiyo, Frank Mwaisumbe alitaja mambo matatu makubwa kutoka kwa Lowassa kuwa la kwanza alihimiza wanachama wote kuimarisha umoja na kufuta mipasuko iliyotokea wakati wa uchaguzi.

Pili, aliwasihi wana Chadema wote kuwa jasiri kwa kupigania haki na kujitambua na la tatu ni kujiandaa kwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika 2019 na Uchaguzi Mkuu wa 2020.

Mwaisumbe alisema baada ya kikao cha jana, leo Lowassa anaanza kutembelea majimbo ambako atakuwa na vikao vya ndani katika majimbo ya Mbeya Vijijini, Mbozi na Tunduma na kesho atakuwa kwenye majimbo ya Nkasi Kaskazini na Kusini na Sumbawanga wakati kesho kutwa atakuwa Mbarali, Makambako, Njombe Mjini na Mafinga. Agosti 25 atakuwa Iringa Mjini na Kolo.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji yupo Kanda ya Serengeti inayojumuisha mikoa mitatu; Simiyu, Shinyanga na Mara na jana aliwataka Watanzania kuwapuuza watu wanaodai chama hicho kimejipanga kufanya vurugu Septemba Mosi akisisitiza kuwa maandamano yatakayofanyika ni ya amani.

Alisema kamwe hawawezi kuvunja sheria na Katiba ya nchi na kwamba kinachofanyika kipo kwa mujibu wa sheria.

 “…Nawaomba Watanzania wote watuunge mkono maana tunachokwenda kukifanya ni kwa ajili ya kuwanusuru watoto wetu wasiingie kwenye matatizo maana kinachoendelea kinakwenda kuondoa demokrasia na utawala bora,” alisema.

Saturday, 20 August 2016

Lissu aibuka kidedea tena mahakamani
 



Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki
By James Magai na Tausi Ally Mwananchipapers@mwananchi.co.tz
IN SUMMARY
Lissu, ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya Chadema  alipandishwa kizimbani Agosti 5, na kusomewa mashtaka matatu, mawili kati yake yakiwa ni ya uchochezi na moja la kuidharau mahakama


Dar es Salaam. Serikali imepigwa mweleka katika kesi ya uchochezi dhidi ya mshtakiwa Tundu Lissu baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutupa pingamizi la Wakili wa Serikali kutaka wakili Peter Kibatala kujitoa kumtetea mwanasiasa huyo.

Lissu, ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya Chadema  alipandishwa kizimbani Agosti 5, na kusomewa mashtaka matatu, mawili kati yake yakiwa ni ya uchochezi na moja la kuidharau mahakama

Tuesday, 16 August 2016


MAISHA SIO FAIR. UFANYAJE KUFANIKIWA?



Kuna mambo mengi yanaweza kuwa wazi kwa mabishano au majibizano. Ila wengi mnaweza weza kukubali kuwa maisha sio fair. Maisha sio fair kwa jinsi wewe unavyoweza kupata milo 3 kwa siku wakati kuwa watu 21,000 wanakufa kila siku kwa sababu ya njaa. Mashuleni madebe ya uchafu yamejaa chakula, na wakati huohuo watu wanachangisha hela zitumwe Somalia kupigana na njaa. Maisha sio fair kwa jinsi kila siku unapita na daladala kuelekea Posta na unapishana na ombaomba huyo huyo kila siku. Mwaka mmoja baadae umenunua gari na bado yule ombaomba yupo na nguo zake zilezile zimechakaa. Maisha sio fair kwa jinsi pesa na kujuana na watu flani zinavyoweza kukufikisha popote pale utakapo, iwe ni umaarufu au hata kazi japokuwa huna maarifa yaliyo bora kupita wengine. Inafurahisha sana kuona familia yenye pesa, watoto wenye akili sana, wazazi wanaojua vitu na watu wakubwa na hivyo wanaweza kuwapatia watoto elimu bora, kuingia vyuo bora duniani na vya gharama bila wasiwasi na kuwahakikishia ajira kupitia watu wanaowajua. Ila fikiria, hii ni fair kwa yule mtoto wa masikini, mwenye akili lakini aliye na wazazi wasiojua vitu au watu wanaoweza kuwasaidia watoto wao kufikia mafanikio?

Lakini japokua maisha yanaweza yasiwe fair, kuna vitu vitatu ambavyo kila mtu anavyo au anaweza kuwa navyo. Haijalishi kuwa ni tajiri au masikini, mtu mzima au mtoto, mwanaume au mwanamke, vitu hivi vitatu vipo kwa wote. Ni hivi vitu ambavyo vinafanya kila kukicha tusikie stori ambazo huonekana kama muujiza. Stori za kama jinsi Bakhresa alivyotoka kuuza viazi vya mviringo mpaka kuwa kati ya matajiri wakubwa Afrika. Stori za kama jinsi Steve Jobs alivyokabidhiwa na wazazi wake kwa watu wengine wamlee mara baada ya kuzaliwa, jinsi alivyoacha kusoma chuo akihofia gharama kubwa na mpaka alivyokuwa mwanzilishi ya kampuni ya Apple, kampuni ambayo imetuletea bidhaa kama Iphone na Ipad. Ni vitu gani hivi?

1. Imani
Kwanza napenda kubainisha kuwa nachoongelea hapa si dini. Nachoongelea hapa ni kuamini kwamba iwe jua au mvua, jambo flani litatimia kwako. Ni kuamini kuwa hakuna kinachoweza kukufanya usifikie ndoto zako kwa kuwa kwako wewe tayari zishatimia. Ni ile Imani ya kuamini wewe ni tajiri wakati una jelo uliyokopa kutoka kwa rafiki yako Juma, ni ile Imani ya kujua ipo siku moja utaheshimika kimuziki kama Diamond wakati una single 5 umeachia na hakuna iliyohit, ni ile Imani ya siku moja na wewe utatajwa sambamba na Ray Kigosi kama kati ya waigizaji bora nchini, wakati huu ni mwaka wa tatu upo chuo cha Sanaa Bagamoyo unahangaika kujua kuigiza (ndoto yako ikitimia usinywe maji mengi lakini). Ni ile Imani ambayo ukimuelezea mtu kitu unachotaka kufanikisha basi atakuona chizi. Imani hii kila mtu anaweza kuwa nayo kama akikitaka kitu flani kwa moyo wake wote. Na ni hii Imani inayomwezesha mtu wa hali duni, mwenye shida na matatizo kibao kuweza kufanya mambo makubwa. Hebu jiulize, ni nini kilichomfanya mtangazaji Millard Ayo atake kuacha masomo ya sekondari na kusomea utangazaji, kama sio Imani kuwa huko ndiko kutamfaa?

2. Bidii
Kwa bahati mbaya sana, hizi sio enzi za Musa ambapo imani yako inaweza kugawanya bahari ili watu wapite. Bidii ya wajenzi itawawezesha wajenge daraja kwa haraka ili watu waweze kupita. Kuwa na Imani pekee haitoshi. Unahitaji kutumia muda na kufanya kazi ili ndoto yako itimie. Inabidi uendelee kusonga mbele hata kama matatizo na majukumu mengineyo yamekuandama bila kusahau kuwa Juma anataka jelo yake aliyokukopesha. Inabidi ujifunze kutosikiliza maneno ya watu wanaokuambia ndoto zako hazina maana hivyo uachane nazo na kufanya mambo ya ‘maana’. Inabidi unaposhindwa ujiinue na kuendelea na safari yako kama kawaida. Aliyegundua balbu alijaribu zaidi ya mara 1000 kuitengeza akashindwa. Na bado akaendelea kujaribu mpaka akapatia. Sasa fikiria, ina maana huyu mtu angekata tamaa alipojaribu mara ya 900 basi leo tusingekuwa na balbu. Hayo ndio maajabu ya bidii, kitu ambacho wewe na mimi tunacho au tunaweza kuwa nacho. Na kutokana na